Saturday, October 13, 2012

Breaking News.RPC wa Mwanza Liberatus Barlow auwawa

Marehemu Liberatus Barlow enzi za uhai wake
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Kamishina Mwandamizi wa Polisi (SACP) Liberatus Barlow ameuawa usiku wa kuamkia leo katika tukio linalohusishwa na ujambazi.

Taarifa kutoka Mwanza ambazo zimethibitishwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema zinasema kuwa Kamanda Barlow aliuawa baada ya kumrudisha dada yake kutoka katika kikao cha harusi ya ndugu yao huko Kitangili.

Kwa mujibu wa Mwema tarai jeshi la Polisi limetuma askali wa kupeleleza maujai hayo na ameomba ushirikinao wa wananchi ili kufanikisha kuwatia mbaroni wahusika wa mauaji.

No comments:

Post a Comment