Sunday, April 22, 2012

Ubabe wa Mfalme Simba katika mbuga ya Serengeti

Mnyama aina ya Simba mpaka leo ndiye anaaminika kuwa mfalme wa pori ambaye maisha yake yote hutegemea kitoweo cha wanyama wengine.Hata hivyo hudaiwa wakati mwingine huzidiwa na kula majani!

Simba huishi kama familia ya baba mama na watoto ambapo mara nyingi Simba jike ndiye mwindaji wakati huo dume hufanya kazi ya kulinda familia na watoto dhidi ya wanyama wengine wanaoweza kuwadhuru..

Maelezo mengine ambayo hayana ushahidi wa kisayansi ni kuwa Simba dume hupenda kubaki nyumbani kulinda mji kutokana na hofu ya kuumia wakati wa uwindaji.Kwa mujibu wa taarifa mbalimbali Simba dume hufikia hadi wastani wa kilo 186 na jike 126.

Simba dume wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wana muda mfupi zaidi wa kuishi ikilinganishwa na Simba jike.Taarifa zinaonyesha kuwa Simba dume katika hifadhi hiyo anaishi hadi miaka 12,ambapo jike hifikia hadi umri wa miaka 15.

No comments:

Post a Comment