Wednesday, August 8, 2012

Wadau wa maendeleo Bukoba wakutana

Phinias Bashaya,Bukoba
 ASKOFU Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba Methodius Kilaini amewashauri wananchi wa Mkoa wa Kagera kubadilika na kutobweteka kuwa maendeleo katika Nyanja mbalimbali hayapatikani bila kuyatolea jasho.

Akichangia katika Mkutano wa wadau wa maendeleo ya Mji wa Bukoba uliofanyika katika ukumbi wa Mtakatifu Fransis alisema mtu anayetafu maendeleo hatakiwi kukata tama hata kama anakumbana na vikwazo mbalimbali katika juhudi zake.

Kiongozi huyo wa kiroho alihusisha kuduma kwa maendeleo ya mji huo na kile alichokiita kuwa ni siasa mfuniko zilizokwamisha mji huo na kupongeza jitihada mpya zinazofanyika kuuboresha na kuvutia shughuli  za kiuchumi.

“Miaka arobaini iliyopita tumekuwa na siasa mfuniko zilizofunika akili za watu,naunga mkono jitihada za kuuondoa na sasa tunatakiwa kusonga mbele,mji umeanza kupanuka na amendeleo lazima uyatolee jasho”alisema Kilaini

Katika Mkutano huo Meya wa Manispaa ya Bukoba Dokta Anatory Aman alisema utekelezaji wa miradi mbali iliyoidhinishwa na Manispaa inalenga kuongeza ajira na kuboresha taswira ya mji huo tofauti na mika mingi iliyopita.

Kwa mujibu wa  Dokta Aman miradi inayotarajiwa kutekelezwa ambayo pia imepata ufadhili ni pamoja na ujenzi wa soko jipya,kituo cha mabasi,jingo la kitega uchumi na upimaji wa viwanja elfu tano katika viunga vya mji wa Bukoba.

Pia Mkutano huo ambao idadi kubwa walikuwa viongozi wa Madhehebu ya dini walikubaliana kuwahamasisha waumini wao kupitia nyumba za ibada umuhimu wa kutunza na kuhifadhi mazingira kwa kila mwananchi kufanya usafi na kupanda miti.

Pia wadau hao walibainisha changamoto mbalimbali zinazoukabili mji wa Bukoba kuwa ni pamoja na ongezeko kubwa la watu lisiloendana na uboreshaji wa huduma kama miundombinu ya maji safi na maji taka.

No comments:

Post a Comment