Thursday, August 9, 2012

Balozi Profesa Mahalu aibwaga Serikali mahakamani

Balozi Profesa Mahalu akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kushinda kesi yake katika mahakama ya Kisutu leo

Waandishi wa habari wakimfuata Balozi Profesa Mahalu akiwa pamoja na Mdogo wake Mirasi Rama wakitoka nje ya Mahakama ya Kisutu Mchana huu mara baada ya kushinda kesi iliyokuwa ikimkabili akidaiwa kununua nyumba ya Ubalozi wa Tanzania nchini Italia, Akisoma hukumu iliyosomwa kuanzia Saa sita leo na Hakimu Mfawidhi mkazi wa mahakama ya Kisutu Mh. Ilivin Mugeta imemtoa Balozi Profesa Mahalu katika hatia na kumwachia huru

Balozi Profesa Mahalu katikati akitoka nje ya mahaka ya Kisutu huku akiwa ameongozana na mdogo wake Mirasi Rama kulia ni Wakili wa kujitegemea Mabere Nyaucho Marando.

Aliyekua Balozi wa Tanzania nchini Italia,Balozi Costa Mahalu alikua mshitakiwa namba moja kwenye kesi ya matumizimabaya ya fedha za ununuzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania nchini Italia, pamoja na mshitakiwa namba mbili Grace Martin  wameshinda leo baada ya  kuonekana hawana hatia yeyote baada ya kukosekana ushahidi wa kuwatia hatiaani.


No comments:

Post a Comment