Sunday, August 5, 2012

Mshauri wa mahakama mbaroni kwa ujambazi

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera SSP Peter Matagi akionyesha bunduki aina ya SMG baada ya kumkamata Mshauri wa Mhakama ya Mwanzo Lusahunga akiwa katika harakati za kwenda kufanya uhalifu.
MSHAURI wa mahakama ya Mwanzo Lusahunga wilayani Biharamulo Mkoani Kagera Enos Kazikie(43)amekamatwa na bunduki aina ya SMG na risasi 248 akiwa katika safari ya kwenda kufanya uhalifu.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera Peter Matagi mtuhumiwa huyo mkazi wa kijiji na Kata ya Nyakanazi alikamatwa tarehe 1,Agosti katika kitongoji cha Kabulaitoke akiwa ameweka silaha hiyo katika buti ya gari.

Alisema polisi wilayani humo walipata taarifa kuwa katika kijiji hicho kuna jambazi anamiliki silaha ndipo ufuatlijai ulipofanyika na mtuhumiwa kunaswa na bundiki na risasi hizo.

Alitaja namba za silaha hiyo kuwa ni SMG 4707,magazine moja na risasi 248 akisema kiasi cha risasi kilichokamatwa ni kikubwa nakama zingeendelea kumilikiwa na majambazi  zingehatarisha maisha ya wananchi na mali zao.

Pia Matagi amesema mbali na kuhusishwa na uhalifu mtuhumiwa huyo inaaminika alikuwa safarini kwenda kuuza siraha hiyo na kuwa msako wa kuwatafuta majambazi wengine waliokuwa wakishirikiana na mtuhumiwa unaendelea.

“Msako wa kuwatafuta majambazi wengine waliokuwa wanashirikiana na mtuhumiwa unaendelea,bunduki alikuwa ameiweka kwenye buti ya gari hata dreva wake gari hilo hakuwa na taarifa”alibainisha Matagi

Kufuatia tukio hilo Kaimu Kamanda Peter Matagi amewataka wananchi Mkoani Kagera kutoa taarifa kwenye vyombo vya usalama wanapotilia shaka mienendo ya baadhi ya wananchi wanaotuhumiwa kujihusisha na uhalifu.

No comments:

Post a Comment