Thursday, May 24, 2012

John Mnyika ashinda kesi ya Ubunge Ubungo

Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika.
Hawa Nghumbi (CCM)
Mbunge wa Jimbo la Ubungo (Chadema), John Mnyika ameshinda kesi iliyokuwa inamkabili ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa  mwaka 2010, baada ya Mahakama kutupilia mbali mashitaka yote matano yaliyokuwa yakimkabili ambayo ni :
1)Kwamba Mnyika alimtuhumu mlalamikaji kuuza nyumba za UWT
2)Kutumia Laptop za Mnyika Kuhesabu kura
3)Kuingia watu wengi wa CHADEMA katika chumba cha kuhesabia kura
4)Kuwepo kwa kura hewa 16,000
5)Kukosewa kwa karatasi za kujumulisha kura (form)

Mlalamikaji Hawa Nghumbi (CCM) anatakiwa kulipa gharama zote za kesi hiyo kama ilivyoamriwa na Mahakama.

No comments:

Post a Comment