Sunday, May 20, 2012

Kombe la Klabu Bingwa Ulaya latua Darajani

Didier Drogba hizi ndiyo zake!
Pamoja na timu ya Chelsea ya Uingereza kutopewa nafasi kubwa ya kunyakua ubingwa mbele ya Bayern Munich waliokuwa katika uwanja wa nyumbani wa(Allience Arena)bado Chelsea walionyesha ubabe na kunyakua kombe la klabu Bingwa ya Ulaya-(champions league) katika uwanjawa ugeneni.
 
Katika mechi hiyo ambayo bingwa alipatukana kwa njia ya matuta baada ya dk 120 wakiwa sare ya goli 1-1. ilikuwa ni Bayern Munich iliyopata goli la kutangulia katika dakika ya 83 kupitia kwa Thomas Muller, dakika tano baadae Didier Drogber aliwainuwa washabiki wa Chelsea kwa kusawazisha goli kwa kuunganisha klosi safi kwa kichwa.hadi dakika 90 matokeo yalikuwa 1-1

Dakika 30 ziliongezwa, ambapo Bayern Munich walikosa penati katika dakika ya 5 ya kipindi cha kwanza cha dakika za nyongeza baada ya Drogba kumwangusha Frank Ribbery, ambapo mshambuliaji wa Bayern Roben alikosa penati hiyo baada ya kipa kuidaka.
Hadi dakika 120 zinamalizika magoli yakabaki 1-1. ndipo penati zikapigwa ambapo Chelsea walipata penati 4 na Bayern penati 3.


No comments:

Post a Comment