Friday, May 18, 2012

Wakuu wapya wa Wilaya za Mkoa wa Kagera waapishwa

Mkuu Mpya wa Wilaya ya Karagwe Darry Rwegasira akila kiapo cha kutumikia nafasi hiyo leo Mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera
Mkuu wa Wilaya mpya ya Kyerwa Luteni Kanali Mstaafu Benedict Kulikila Kitenga akila kiapo cha kuwa kushika majukumu ya kuongoza wilaya hiyo leo asubuhi 
Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Mstaafu Issa Suleiman Njiku akila kiapo cha kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo.Katika uteuzi uliofanyika hivi karibuni Njiku hakukumbwa na mabadiliko na kuendelea kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo

Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Kagera walioapishwa leo na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe.Kutoka Kushoto waliokaa  Zipola Pangani(Bukoba)Luteni Kanali Mstaafu Benedict Kitenga(Kyerwa)Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe,Costantine Kanyasu(Ngara),Kanali Mstaafu Issa Njiku(Missenyi),Mkuu wa Mkoa Mstaafu Jenerali Tumainieri Kiwelu.Waliosimama kutoka kushoto Richard Nyamweli Mbeho (Biharamulo)Darry Rwegasira(Karagwe)na Limbres Kipuyo (Muleba).

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Samwei Kamote (kulia)ambaye ameachwa katika uteuzi uliofanyika akipongezwa na Zipora Pangani Mkuu Mpya wa Wilaya hiyo aliyerithi nafasi yake.Katika sherehe hizo Kamote ametajwa kama mfano wa viongozi wenye heshima ya utumishi uliotukuka baada ya kufanya kazi hiyo kwa muda mrefu na mafanikio

Baadhi ya viongozi wa madhehebu mbali mbali ya dini wakifuatilia zoezi la kuwaapisha wakuu wapya wa Wilaya za Mkoa wa Kagera
Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM)Wilaya ya Bukoba Magreth Abuhoro akisalimiana na Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Kagera Bwana Fumbuka baada ya kuapishwa kwa wakuu wapya wa Wilaya
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Costansia Buhiye akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuapishwa kwa wakuu wapya wa Wilaya za Mkoa wa Kagera.Kushoto kwake ni Askofu wa Jimbo Kathoriki la Bukoba Baba Askofu Nestory Timanywa
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Jenerali Tumainieri Kiweru ambaye wakati wa kutambulishwa aliitwa kwa jina la 'Afande'akifuatilia kwa umakini uapishaji wa Wakuu wapya wa Wilaya za Mkoa wa Kagera
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe amewataka wakuu wapya wa Wilaya kupambana na umasikini wa kipato katika maeneo yao ili kuinua pato la Mkoa wa Kagera.

Katika hotuba aliyoitoa mara baada ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya walioteuliwa hivi karibuni,Kanali Masawe amesema ni aibu mkoa wa Kagera kuwa katika nafasi ya 19 kwa kiwango cha umasikini ikilinganishwa na mikoa mingine.

Amewataka kuongeza pato la Mkoa wa Kagera kwa kusimamia shughuli za kilimo chenye tija huku akiwaonya wananchi wanaoendekeza uzurulaji na ulevi badala ya kutumia muda huo katika shughuli za uzalishaji.

Katika sherehe za kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya zilizofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pia Knali Massawe amewataka viongozi na wananchi kutembelea vivutio mbalimbali katika wilaya za Mkoa wa Kagera kama njia ya kuvitangaza.

Akitoa shukrani kwa niaba ya wakuu wapya wa wilaya walioapishwa,Mkuu wa wilaya ya Missenyi Kanali Issa Njiku amesema watazingatia maelekezo waliyopewa na kuhaidi kufanya kazi kwa kushirikiana na viongozi wengine katika maeneo yao ili kufikia lengo la kurudisha heshima ya Mkoa wa Kagera katika shughuli za kiuchumi na kijamii kama ilivyokuwa baada ya Uhuru.

No comments:

Post a Comment