Wednesday, May 2, 2012

Mahakama yatupa pingamizi dhidi ya uchaguzi Mkuu wa KCU (1990)LTD


Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa KCU wakiwa katika kutano wao wa kawaida wiki iliyopita ambapo pamoja na mambo mengine ulipitisha malipo ya pili ya kahawa kwa wakulima
Meneja Mkuu wa KCU Vedasto Ngaiza(wa kwanza kulia)anayefuata ni Mwenyekiti wa Bodi ya Chama hicho John Binunshu wakiwa katika Mkutano uliomalizika wiki iliyopita
MAHAKAMA ya hakimu mkazi wa Bukoba imetupilia mbali  pingamizi lilowekwa  la kuzuia kufanyika kwa  mkutano mkuu wa chama cha ushirika cha Kagera (KCU 1990) ulioandaliwa kwa ajili ya kuichagua bodi mpya ya wakurugenzi ya chama hicho na kutangaza mapendekezo ya bei mpya ya ununuzi wa kahawa kwa msimu wa mwaka 2012.

Hukumu hiyo imetolewa na hakimu mkazi wa mahakama ya Mkoa wa Kagera,na kutupilia mbali pingamizi  la kuzuia mkutano mkuu utakaofanyika mei  3, mwaka huu  lililokuwa limewasilishwa katika mahakama hiyo  na Diocress Rutabana na Sued Juma Kagasheki  wakisimamiwa  na wakili maarufu mkoani Kagera Josephat Rweyemamu.

Rutabana na Kagasheki walikuwa  wameweka pingamizi la mkutano huo kwa madai kwamba baadhi ya  wawakilishi wa mkutano huo mkuu wa cha hicho sio halali, walikuwa wakidai kuwa kila chama cha msingi kinachounda chama cha ushirika mkoani Kagera kuwa  kinapaswa kuwasilishwa na  wajumbe wawili wawili na wala sio ya wajumbe watatu toka katika chama cha ushirika.

Mashauri aliiambia mahakama hiyo kuwa pingamizi hilo lililokuwa limewekwa kwamba sio sahihi hivyo aliamuru taratibu za maandalizi ya mkutano mkuu wa chama cha ushirika mkoani Kagera uendelee na akasema kuwa kama walalamikiaji hawaridhiki na maamuzi yaliyotolewa wanaweza kukata rufaa katika ngazi nyingine.


No comments:

Post a Comment