Monday, May 28, 2012

Madiwani wa Missenyi watimuliwa kwenye majengo ya Saccos


Aliyewahi kuwa Mbunge wa Nkenge Balozi Dkt Diodorus Kamala akizindua Chama cha Kuweka na Kukopa (Saccos)katika Kata ya Buyango ambapo wakati wa kipindi chake alijenga majengo ya Ofisi hizo kwa kila Kata.Picha hii ilipigwa mwaka jana
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM)kimewataka madiwani wa Wilaya ya Missenyi Mkoani Kagera wanaotumia majengo ya vyama vya kuweka na kukopa(Saccos)kama ofisi zao kuondoka katika majengo hayo.

Agizo hilo lilitolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Nape Nnauye siku ya Ijumaa baada ya kupokea malalamiko ya Umoja wa Vijana wa chama hicho(UVCCM)waliodai baadhi ya madiwani wamegeuza majengo ya Saccos kwa ajili ya matumizi ya ofisi zao.
Nape alikuwa Wilayani humo kufungua Baraza la vijana wa UVCCM ambalo pia lilihudhuriwa na wanachama wa chama hicho na viongozi mbalimbali huku kukiwa na mwitikio mdogo wa vijana.
Nape aliwataka madiwani hao kujenga ofisi zao na kuwa wanatakiwa kuondoka katika majengo hayo na kuwa wasisubiri vijana waendelee kulalamikia suala hilo linaloathiri ukuaji wa vyama hivyo.
"Madiwani jengeni ofisi zenu acheni zifanye kazi ya Saccos,kama madiwani mliweza kushawishi wapiga kura wakawachagua tushawishi pia tukujengee ofisi"alisema Nape
Aidha Nape alisema endapo madiwani hao wataendelea kutumia majengo ya Saccos kama ofisi zao wanaweza pia kuhatarisha ukuaji  na lengo zuri la kuanzisha wa vyama hivyo vya kuweka na kukopa.
Awali Katibu wa UVCCM Wilayani Missenyi Philbert Ngemera katika taarifa yake kwa Nape alisema majengo ya Saccos yalioyengwa kila Kata na aliyekuwa mbunge wa Jimbo hilo Dk Diodorus Kamara yametekwa na baadhi ya madiwani na kuzifanya kuwa ofisi zao.
Pia alihainisha changamoto mbalimbali zinazowakabiri vijana  kuwa ni pamoja na upandaji holela wa bidhaa na vijana kukimbia chama hicho kwa madai ya kutowajali huku wakiendelea kuwa na maisha magumu.
Aidha alisema katika baadhi ya maeneo wamekosa vijana wakujitokeza kugombea uongozi kwa kile alichodai ni wengi wao kukosa sifa na kuwa hadi sasa vijana 178 wamekimbia chama hicho na kuhamia Chadema idadi aliyosema ni ndogo ikilinganishwa na vijana wengi wanaoendelea kuiunga mkono CCM.
Kaatika hotuba yake pia Nape aliwaeleza vijana kuwa wana nafasi ya kuchagua viongozi wanaofaa kukiimarisha chama na kuwa wasikubari kurubuniwa hasa katika kipindi hikia mbacho CCM inaendelea na uchaguzi wa ndani.
Mbali na kusema kuwa mageuzi ni lazima ndani ya chama hicho ili kuendana na wakati pia alisema hata wakuu wa Wilaya walioteuliwa hivi karibuni chama kimewaeleza wasifanye mchezo katika maeneo yao kwani nyumbani kwao ni CCM.
Kwa mujibu wa Nape wakuu hao wa wilaya wanatakiwa kufanya kazi kwa masirahi ya chama na kuongeza kuwa ikitokea chama kingine kinachukua dola nacho kinachagua viongozi wake.

No comments:

Post a Comment