Monday, April 23, 2012

Chadema yateka ngome ya CCM Missenyi

Baadhi ya akina mama na watoto katika kijiji cha Burifani ulipo mji wa Kyaka wilayani Missenyi wakifanya biashara ya ndizi za kuchoma na mahindi, wateja wao wakubwa wakiwa ni abiria wanaosafiri kati ya miji wa Bukoba,Karagwe na mpaka wa Mutukula
 Missenyi

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema)kimeshinda uchaguzi wa Mwenyekiti wa kijiji cha Burifani Kata ya Kyaka Wilayani Missenyi ambacho ni makazi ya vigogo wa CCM akiwemo Mbunge wa Jimbo la Nkenge Ansupter Mshama.

Mgombea wa Chadema Deogratias Laurian aliibuka na kura 401 dhidi ya 129 za mgombea wa CCM Mathias Kibarwiga. Mgombea wa TLP Plasid Vedasto akiambulia kura 2,ambapo wakati wa kutangaza matokea Msimamizi Msaidizi Magreth Kamya alisema kura 4 ziliharibika.

Pia katika maeneo mbalimbali ya mji wa Kyaka ambao upo kijiji cha Burifani ulitawaliwa na askali polisi na mgambo waliokuwa wamejihami kukabiriana na vurugu zozote ambazo zingetokea.

Vigogo wengine wa CCM wanaotoka katika kijiji hicho ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Fidelis Kibarabara,Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Missenyi ambaye pia ni Diwani wa Kata hiyo,Projestus Tegamaisho,Katibu wa Jumuiya ya Vijana na Katibu wa UWT,ambapo pia Ansupter Mshama ni Mwenyekiti wa UWT.

Uchaguzi huo ambao ulifanyika jana Jumapili awali ulitawaliwa na mizengwe kwa mgombea wa Chadema kuwekewa pingamizi na upande wa CCM wakimtuhumu kwa vitendo vya rushwa na hivyo uchaguzi kuhairishwa mara mbili.

Hata hivyo pingamizi dhidi ya tuhuma za rushwa hazikuwa na uthibitisho na kutupiliwa mbali na Msimamizi wa uchaguzi wa Wilaya Issaya Mbenje ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri.

Miongoni mwa sababu zinazotajwa kukiponza Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi huo ni kero za vizuizi vinavyodaiwa kuwanufaisha baadhi ya viongozi, na mgogoro wa kiwanja cha Msikiti unaodaiwa kuingiliwa na kiongozi mmoja wa Wilaya.

Pia miongoni mwa sababu zilizompa ushindi mgombea wa Chadema ni wananchi kupigwa danadana kuhussu malipo ya fidia ili kupisha ujenzi wa barabara ya Kyaka Bugene inayojengwa kwa kiwango cha lami.
 
 
 
 
 
 

No comments:

Post a Comment