Thursday, April 19, 2012

Ubeligiji yatumia Bilioni 120 kuboresha zao la migomba Mkoani Kagera

Ngara
Shirika la Maendeleo la Ubeligiji(BTC)kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania limetumia zaidi ya shilingi bilioni 120 kwa ajili ya mradi wa migomba unatekelezwa katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera na Wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma.

Hayo yamebainishwa na Ofisa Mradi huo Bwana Cranme Chiduo wakati wa maadhimisho ya siku ya zao la ndizi yaliyofanyika katika kijiji cha Rusumo wilayani Ngara ambayo yamefunguliwa rasmi na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massaawe.

Amesema tangu Mradi huo uanzishwe miaka minne iliyopita mbali na kutumia kiasi hicho cha fedha pia umepata mafanikio makubwa katika usambazaji wa mbegu bora za migomba na kuwasaidia wasindikaji na wasambazaji kuongeza thamani ya zao la ndizi.

Mratibu wa Mradi wa migomba unaofadhiliwa na Serikali ya Tanzania na Ubeligiji Mgenzi Byabachwezi akitoa maelezo ya jinsi ya kudhibiti magonjwa yanayoshambulia migomba kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe alipotembelea shamba la kikundi cha Mshikamano Kata ya Magoma Wilayani Ngara leo asubuhi
Mwenyekiti wa Mtandao wa Vikundi vya Usindikaji wa Mazao ya Wilayani Missenyi(MVUMI)Bwana Fredrick Kitone akionyesha ustadi wa kumenya ndizi kwa ajili ya kuzianika na kuandaa makopa ambayo hutoa unga unaotumika kwa ajili ya ugali unaotokana na ndizi
Katika maadhimishisho hayo Mratibu wa Mradi wa Migomba Mkoani Kagera Mgenzi Byabachwezi amesema hadi Desemba mwaka jana zaidi ya miche bora ya migomba milioni mbili imesambazwa kwa wakulima 45,843 katika maeneo unapotekelezwa mradi huo.

No comments:

Post a Comment