Sunday, April 22, 2012

Rais Jacob Zuma tena

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini akiwa katika vazi la asili la Kabila lake wakati wa sherehe za kuoa mke wa nne
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ameoa mke wa nne, kwenye sherehe ya jadi ambapo wake zake wengine watatu pia walihudhuria sherehe hizo.
Zuma mwenye umri wa miaka 70, alivaa ngozi ya chui na kubeba mkuki na ngao, mavazi ya jadi ya Kizulu, kwenye harusi iliyofanywa jimbo la KwaZulu-Natal.
Bi arusi, Bongi Ngema, amefuatana na Rais Zuma kwenye ziara zake rasmi kwa miaka kadha ambapo imedaiwa sherehe hizo zimegharimiwa na Zuma mwenyewe.Rais Zuma ni mtu anayefuata mila za kabila lake la Zulu.
Mwenyewe amezaliwa na baba aliyekuwa na wake kadha na ndoa yake kwa Bi Ngema ni ya sita.Mmoja, ambaye ni waziri wa serikali, alimuacha naa mwingine alijiua.
Nyumba ya Rais Zuma imetengenezwa kwa ustadi na ukubwa wa kutosha ili kuweza kukidhi mahitaji ya familia yake ambapo inaaminika ana watoto zaidi ya ishirini.

No comments:

Post a Comment