Tuesday, April 24, 2012

Mkutano wa KCU ulivyofanyika leo mjini Bukoba

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika Mkoa wa Kagera John Binushu akijadiri jambo na Mrajisi wa Vyama Vya Ushirika Mkoani Kagera Rwenkiko Shorosi
Mjumbe kutoka Chama Cha Msingi Rukurungo Charles Kihima kwa umakini mkubwa akipitia kabla wakati wa mkutano wa KCU  uliofanyika leo
Mzee Super Kalugaba Mwenyekiti wa Chama Cha Msingi Kamachumu kisisitiza uboreshaji wa Hotel ya Lake na kuonyesha mashaka juu ya usimamizi wa Hotel hiyo
Mwanasheria kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Dk Audax Rutabanzibwa naye amehudhuria Mkutano huo
Mjumbe kutoka Chama Cha Msingi Ibwera Wilaya ya Bukoba Vijijini Sadru Nyangasha akichangia moja ya hoja zilizojitokeza wakati wa Mkutano
Mjumbe kutoka Kmachumu Archard Muhandiki akitoa maoni ya kuboresha Hotel ya Lake inayomilikiwa na KCU ambayo wajumbe wametuhumu usimamizi mbaya unaosababisha iendeshwe kwa hasara inayomrudia Mkulima
Mkutano wa Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Kagera(KCU)umefanyika leo mjini Bukoba katika Hotel ya COOP inayomilikiwa pia na Chama hicho kinachoundwa na vyama vya  msingi vya Wilaya za Muleba,Missenyi na Bukoba.

Mkutano huo uliokuwa unajadiri hesabu za Mizania na Mapato,wajumbe  pamoja na mambo mengine walishangazwa na taarifa za Hotel ya Lake inayomikikiwa na KCU kupata faida ya shilingi milioni moja baada ya kuwekeza milioni 87 kwa mwaka uliopita.

No comments:

Post a Comment