Monday, April 23, 2012

Mliosoma Ihungo Sekondari

Historia inawataja Askofu wa Jimbo Kathoriki la Bukoba Nestory Timanywa,Mwenyekiti wa CHADEMA,Freeman Mbowe na aliyewahi kuwa Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Dk Diodorus Kamala.
Pia Waziri wa Nishati na Madini William Ngereja,mhadhili wa chuo Kikuu cha Dar es salaam Ally Bashiru na mamia ya wengine katika nyanja tofauti tangu mwaka 1929.
Sifa pekee inayoitofautisha na shule nyingine kongwe hapa nchini ni mafanikio ya mwaka 1968 wanafunzi wake walipoongoza katika matokeo ya mitihani miongoni mwa shule za Jumuiya ya Madola.
Maabara ya kemia enzi hizo ilijenga kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi 18,hivi sasa inatakiwa kutumiwa na wanafunzi 176 na hivyo kusababisha changamoto kubwa kwa walimu na wanafunzi.
“Maabara ya kemia ina uwezo wa kutumiwa na wanafunzi 18 hii ni changamoto kubwa inayosababisha utendaji kuwa mdogo”anafafanua mwalimu wa somo la Kemia Tumwesige Philemon

No comments:

Post a Comment