Monday, April 23, 2012

Wananchi walioiliza Kamati ya Profesa David Mwakyusa

Moja ya familia katika Kitongoji cha Kazizi Kijiji cha Bubare Wilayani Missenyi ambayo haina makazi baada ya nyumba yao kubomolewa kufuatia mgogoro unaoendelea kufukuta kati ya wananchi na wawekezaji
Mwanamke katika kitongoji cha Kazizi akiwa nje ya mabaki ya nyumba yake ikiwa ni sehemu ya nyumba 36 zilizoteketezwa moto wananchi wakishinikizwa kuwapisha wawekezaji.Mama huyu pia anaonekana ni shabiki wa Arsenal
Wanafunzi katika Kijiji cha Bugango Wilayani Missenyi ambao wameathiriwa na mgogoro kati ya wananchi na wawekezaji
Faustin Mukasa,mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya Sekondari Bugango akiwa na kovu la risasi aliyopigwa kwa madai ya kukatiza katika eneo la Mwekezaji wakati akienda shule

Jana kabla ya kuhairishwa kwa kikao cha Bunge,Kamati ya Mifugo Kilimo na Maji ilitoa taarifa ya kile ilichoshuhudia baada ya kutembelea maeneo yenye migogoro kati ya wananchi na wawekezaji kwenye lanchi zilizoko Mkoani Kagera.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Profesa David Mwakyusa alisema mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo alitoa machozi baada ya kujionea hali halisi katika lanchi za Missenyi na ukiukwaji mkubwa wa haki za Binadamu.
Moja ya mapendekezo ya Kamati hiyo kwa Serikali ni kurudiwa kwa mipaka na kuwa wawekezaji ambao wanaishi nje ya nchi bila kuendeleza maeneo yao huku wakiendesha unyanyasaji kwa wananchi wanyang’anywe maeneo yao.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda alisema Serikali itazingatia mapendekezo na ushauri.Tume ilifika  Kagera mwezi Februari ikiongozwa na Neema Mgaya(Viti maalumu Vijana CCM) akiambatana na Titus Kamani(Busega)Seleman Jafo(Kisarawe)Waride Jabu na Asaa Hamad wote kutoka Zanzibar.

No comments:

Post a Comment